This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Monday, 31 December 2012

PENDEKEZO LA RAIS BOZIZE LAKATALIWA NA WAASI WA CAR

Rais wa CAR akiwahutubia wanainchi mjini Bangui
Waasi nchini Jamuhuri ya Afrika ya Kati, wamekaribia mji mkuu wa nchini Bangui na wamepuuzilia mbali, tangazo la rais wa nchini hiyo Francois Bozize, siku ya Jumapili, kuanzisha mazungumzo ya amani na viongozi wao.
Msemaji wa waasi wa Eric Massi, ameiambia BBC kuwa, ni vigumu sana kwao kumuamini rais Bozize, kwa sababu wanajeshi wake wanaendelea na harakati za kuwashambulia wapiganaji wao mjini Bangui
.
Amesema, ikiwa jeshi la kutunza amani la Muungano wa Afrika , halitatumwa mjini Bangui, waasi hao wataingia na kutoa ulinzi wa wafuasi wao.
Lakini serikali ya nchi hiyo imekanusha madai hayo, ya kuwafanya mashambulio dhidi ya wafuasi wa waasi hao.
Siku ya Jumapili, rais Bozizi alitangaza kuwa yuko tayari kuunda serikali ya muungano wa kitaifa na waasi hao na kuwa hatawania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2016.
Share:

WATU WAWILI WAUAWA BAADA YA KANISA KUSHAMBULIWA....


Viongozi wa Kanisa la Coptic
Raia wawili wa Misri wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa, kwenye shambulio liliotekelezwa dhidi ya kanisa moja la Coptic mjini Misrata.

Afisa mmoja wa baraza la mji huo amesema kuwa kumetokea mlipuko ndani ya jengo la kanisa hilo wakati wanne hao walipokuwa wakila chakula chao cha mchana.

Haijulikani ni nani aliyefanya shambulio hilo mjin Dafiniyah, viungani wa Misrata.
Hata hivyo kuna habari za kutatanisha kuhusu ni lini shambulio hilo lilitokea.
Share:

Sunday, 30 December 2012

MWILI WA MWANAMKE ALIYEBAKWA INDIA KURUDISHWA ,WAZIRI MKUU ASIKITIKA UNYAMA HUO


na abdul mtulya


epa03518670 An Indian protester holds a candle and others placards, during a silent protest march held by sex workers, transgender and gays, against the gang rape of a student in New Delhi a week back, in Mumbai, India, 27 December 2012. The 23 year old woman who was gang-raped by 6 men on a moving bus on the night of 16 December 2012 has been flown to a Singapore hospital for further treatment of her severe internal injuries. EPA/DIVYAKANT SOLANKI

Wanawake wakiandamana nchini India wakipinga matumizi ya nguvu katika ngono

Indian Prime Minister Manmohan Singh attends a Full Planning Commission meeting at his residence in New Delhi on September 15, 2012. Indian Prime Minister Manmohan Singh defended September 15 a string of economic reforms unveiled by his government, despite protests over higher fuel prices and new foreign investment rules. AFP PHOTO/POOL/RAVEENDRAN (Photo credit should read RAVEENDRAN/AFP/GettyImages)
waziri mkuu wa india manmohan sing


Mwili wa mwanamke wa India ambaye amefariki hospitalini nchini Singapore baada ya kubakwa kinyama mjini New Delhi umerejeshwa kwa ndege maalum ya kukodi jana Jumamosi(29.12.2012).
Balozi  wa  India  nchini  Singapore T.C.A Raghavan  amewaambia waandishi  habari, saa  kadha  baada  ya  mwanamke  huko  kufariki kutokana  na  viungo  vyake  kushindwa  kufanya  kazi  katika hospitali  nchini  Singapore  ambako  alikuwa  akipatiwa  matibabu.
Mwanamke  huyo  na  ndugu  wa  marehemu  watasafirishwa kwenda  India   katika  ndege  maalum  ya  kukodi  baadaye  mchana wa  leo  Jumamosi, (29.12.2012) , amesema  Raghavan.

Waziri mkuu  ahuzunika

Waziri  mkuu  wa  india  Manmohan Singh  amesema   kuwa amesikitishwa  sana  na  kifo  cha  mwanamke  huyo  ambaye alifanyiwa  vitendo  vya  kinyama  kwa  kubakwa  na  kundi  la  vijana na  kwamba  maandamano  yaliyozuka  kutoka  na  kitendo  hicho , "yanaeleweka".
"nimesikitishwa  mno  kufahamu  kuwa  mhanga  huyo  wa mashambulizi  ya  kinyama  ambayo  yalifanyika  Desemba 16  mjini New Delhi  ameshindwa kunusurika  kutokana  na  majeraha makubwa  aliyoyapata  baada  ya  shambulio dhidi  yake, " ameandika  waziri  huyo  mkuu  katika  tovuti  yake.
"Tumekwisha  ona  hisia  na  nguvu  ambazo  tukio  hili limesababisha. Hii  ni  hali  ambayo  inaeleweka  kutoka  kwa  vijana wa  india  ambao  wanataka  mabadiliko  ya  kweli.
"Nataka  kuwaambia , familia  yake  na  taifa  kwa  jumla  kuwa amepoteza maisha,  ni  juu  yetu  wote  kuhakikisha  kuwa  kifo chake  hakitakuwa  cha   bure."
Indian Prime Minister Manmohan Singh attends a Full Planning Commission meeting at his residence in New Delhi on September 15, 2012. Indian Prime Minister Manmohan Singh defended September 15 a string of economic reforms unveiled by his government, despite protests over higher fuel prices and new foreign investment rules. AFP PHOTO/POOL/RAVEENDRAN (Photo credit should read RAVEENDRAN/AFP/GettyImages) Waziri mkuu wa India Manmohan Singh
India  imetikiswa  na  maandamano  makubwa  tangu  msichana huyo  mwenye umri  wa  miaka 23 kushambuliwa  kinyama  katika basi  mjini  New Delhi  na  kundi  la  watu  sita.
Serikali  imekuwa  ikijaribu  kulituliza  wimbi  la  hasira  kwa  kuahidi adhabu  kali kwa  uhalifu   mkubwa  unaohusiana  na  ngono  pamoja na  kuunda  tume  maalum  ya  uchunguzi  kuhusiana  na  jinsi  ya kushughulikia  kesi  za  ubakaji.

Polisi wautaka  umma  kuomboleza kwa amani

Police detain a demonstrator in front of the India Gate during a protest in New Delhi December 23, 2012. The Indian government moved on Sunday to stamp out protests that have swelled in New Delhi since the gang-rape of a young woman, banning gatherings of more than five people, but still thousands poured into the heart of the capital to vent their anger. REUTERS/Adnan Abidi (INDIA - Tags: CRIME LAW CIVIL UNREST TPX IMAGES OF THE DAY)
Polisi wanajiandaa kwa maandamano makubwa zaidi nchini India


 Wakati maafisa  wakijitayarisha  kwa  ghasia  zaidi mitaani, polisi wameonekana  kuongezwa katika  eneo  la  kati  la  mji  mkuu  wa india   kabla  ya  mwili  wa  msichana  huyo  mwenye  umri  wa miaka  23 haujarejeshwa  nchini  humo. Afisa  wa  polisi  wa  mjini New Delhi  amehimiza  watu kuomboleza  kifo  cha  mwanamke  huyo kwa  amani  wakati  maeneo  kadha  ya  mji  huo mkuu  yamefungwa.
Singh , ambaye  hapo  kabla  alitoa  wito  wa  utulivu , amesema kuwa  itakuwa , "Heshima  kubwa  kwa  kumbukumbu  yake  iwapo tutaweza  kuelekeza  hisia zetu hizi  na  nguvu  katika  kuchukua hatua  sahihi."
"Kwa  muda  huu tunahitaji  mjadala  wa  maana  na  uchunguzi kuhusiana  na  mabadiliko  ya  lazima  na  haraka  ambayo yanahitajika  katika  mtazamo  wa  jamii.
"Ni  matumaini  yangu  kuwa  tabaka  lote  la  kisiasa  pamoja  na jamii yote  itatenga maslahi  yao  finyu  ya  binafsi  na  ajenda  ili kutusaidia  kufikia  hatima  ambayo  tunaikusudia, na  kuifanya  india kuwa  mahali  bora  na  salama  kwa  wanawake  kuweza  kuishi.
Share:

Profesa Shivji umepotoka kuponda kesi ya Lema Lissu asema



mwanazuoni wa siku nyingi nchini, Profesa Issa Shivji
Share

Na Fredy Azzah
HATUA ya mwanazuoni wa siku nyingi nchini, Profesa Issa Shivji kupinga hukumu ya Mahakama ya Rufani Tanzania iliyomrejeshea ubunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema imemtia matatani na baadhi ya watu wanasema gwiji huyo wa sheria “huenda amenukuliwa vibaya au hajasoma hukumu husika.”
Jana Wakili wa Lema, Tundu Lissu, alimkosoa Profesa Shivji pamoja na Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, Francis Stolla akisema wanasheria hao wamepotoka katika matamshi yao ya kupinga hukumu ya Mahakama ya Rufani.
Matamshi ya Shivji pia yaliiteka mijadala katika mitandao ya kijamii ya Jamii Forums, Mabadiliko na Facebook ambako wachangiaji  walikuwa wakivutana huku baadhi yao wakisema wazi kwamba msomi huyo amekosea huku wengine wakimtetea kwamba yuko sahihi.
Akizungumza na gazeti hili jana kutoka Songea mkoani Ruvuma, Lissu alipinga vikali hoja zilizotolewa na Profesa Shivji pamoja na Stolla, akisema kuwa hazina mashiko na zinaweza kutolewa tu na mtu ambaye hakufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.
Juzi Profesa Shivji na Stolla walinukuliwa wakiikosoa hukumu ya Mahakama ya Rufani, iliyomrejesha bungeni Lema wakisema hukumu hiyo iliyotolewa na majaji watatu Salum Massati, Bernard Luanda na kiongozi wao Nathalia Kimaro, inapingana na sheria.
Lissu katika maelezo yake alisema uamuzi wa mahakama katika kesi ya Lema umejenga upya msingi bora wa matumizi ya vyombo vya uamuzi, kwani kesi nyingi za kupinga matokeo ya ubunge, zimekuwa zikifunguliwa na watu ambao wamekuwa wakitumwa na vigogo wa kisiasa na watu wenye fedha.
Akizungumza na Mwananchi, Lissu alisema hoja hizo hazina mashiko na kuwa ile iliyotolewa na Profesa Shivji inatokana na msomi huyo kuzungumza kitaalamu bila kuangalia mazingira halisi ya siasa za Kitanzania.
Lissu alisema mahakama ya rufani haikupiga marufuku wapiga kura kufungua kesi za kupinga ila iliwataka tu kufanya hivyo pale haki zao zinapokiukwa.
“Kwanza siyo kweli kwamba mahakama imepiga marufuku wapiga kura kufungua kesi, ilisema watafanya hivyo pale ambapo haki zao zimevunjwa, haki zenyewe ni kupiga kura, kura zao kutohesabiwa ama suala jingine litakalomnyima kupiga kura, hizo ndiyo haki za mpiga kura,” alisema na kuongeza:
“Sasa mwalimu wangu, Profesa Shivji yeye anatazama tu kwa jicho la kitaalamu na kusema haki za binadamu zimekiukwa, kwa muda wanasiasa, matajiri na CCM wamekuwa wakiwatumia wananchi kuwapinga wabunge wa upinzani.”
Uchambuzi wa Lissu
Alitoa mfano akisema katika uchaguzi wa 1995, Dk Willibrod Slaa alishinda ubunge na watu wanaojiita wananchi walifungua kesi kupinga ushindi huo, mwaka 2000 wakampinga tena na hata 2005.
Alisema 1995 Makongoro Nyerere aliposhinda ubunge katika Jimbo la Arusha Mjini kupitia NCCR- Mageuzi, watu wanaojiita wananchi walifungua kesi ambayo matokeo yake yalikuwa mbunge huyo kupoteza kiti chake.
Lissu alisema 2005 aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Marehemu Chacha Wangwe alifunguliwa kesi na watu waliojiita wananchi ambao mwisho wake walishindwa.
Share:

Saturday, 29 December 2012

Matatani Wafanyakazi Tanroads kwa rushwa


 
TAASISI ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Morogoro, imewafikisha mahakamani wafanyakazi watatu wa wakala wa Barabara Nchini (TANRODS) wa kituo cha mizani cha Mikese mkoani hapa kwa tuhuma za kuomba rushwa ya Sh40,000.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mkuu wa taasisi hiyo Mkoa wa Morogoro, Stella Mpanju tukio la kuwafikisha katika mahakama ya wilaya ya Morogoro watuhumiwa hao lilifanyika Desemba 13 ambapo kesi ilitajwa kwa mara ya kwanza na inatarajiwa kusikilizwa tena leo.
Mpanju alisema watuhumiwa hao ambao ni Happiness Minja (29), Victor Mongi (30) na Eliud Mwakamela (29) walifikishwa mahakamani hapo baada ya kuvunja sheria ya kutoa na kupokea rushwa kifungu cha 15 (10)(a) namba 11 ya mwaka 2007.
Alisema washtakiwa hao walikamatwa Desemba 10, baada ya mshtakiwa kwanza, Happiness Minja, kudaiwa kuomba hongo ya Sh40,000 kutoka kwa dereva wa lori ambalo lilikuwa limezidisha uzito na fedha hizo kudaiwa kugawiwa kwa wafanyakazi wote watatu.
Kutokana na tukio hilo mkuu huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro ametoa wito kwa wananchi hususan madereva kutoa taarifa za vitendo vya rushwa vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wasio waadilifu wa mizani za Mikese, Kihonda na Mikumi ili hatua ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Share:

Friday, 28 December 2012

FERGUSON NA PARDEW WAZOZANA

28 Disemba, 2012 
Sir Alex Ferguson
Sir Alex Ferguson

Kocha wa Manchester Sir Alex Ferguson amemshutumu kocha wa Newcastle Allan Pardew na kumtaja kuwa mfarisayo na mnafiki.
Pardew alimshutumu Ferguson kwa utovu wa nidhamu baada ya mechi yao siku ya jumatano.
Pardew amesema shirikisho la mchezo wa soka nchini England, FA lingemuadhibu Ferguson kwa kukabiliana na maafisa waliokuwa wakisimamia mechi hiyo ambayo Manchester United ilishinda kwa magoli 4-3, katika uwanja wa Old Trafford.
'' Allan Pardew ndiye kocha ambaye mara nyingi huwazomema marefa kwa takriban karibu mechi zote'' alisema Ferguson.
Pardew alipigwa marufuku ya kutohudhuria mecho mbili baada ya kupatikana na hatia ya kumsukuma mmoja wa wasimamizi wa mechi yao mwezi Agosti.
Ferguson alimzomea refa wa mechi hiyo Mike Dean, naibu wake Jake Collin na Neil Swarbrick, mwanzo wa kipindi cha pili ya mechi yao ya ligi kuu ya Premier kupinga goli la pili la Newcastle.
Dean aliidhinisha kuwa Papiss Cisse, hakuwa ameotea wakati Jonny Evans alipojifunga kunako dakika 28.
Share:

UPINZANI MAHAKAMANI KUPINGA MATOKEO NCHIN GHANA

 28 Disemba, 2012 - Saa 15:28 GMT
Nana Akufo Addo
Kiongozi wa NPP Nana Akufo
Chama kikuu cha Upinzani nchini Ghana kimewasilisha kesi katika mahakama kuu zaidi nchini humo kupinga ushindi wa rais John Mahama katika uchaguzi wa urais uliofanyika mapema mwezi huu.
Chama cha National Patriotic Party (NPP) kimepinga matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika tarehe Saba Desemba, ikidai ulikumba na udanganyifu mkubwa.
Tume ya uchaguzi nchini humo ilisema kuwa Bwana Mahakama alipata asilimia 50.7 ya kura zote zilizopigwa, idadi ambayo ni kubwa na hivyo kuepuka duru ya pili ya uchaguzi dhidi ya mgombea wa chama cha NPP Nana Akufo-Addo, ambaye alipata asilimia 47.7 ya kura.
Waangalizi wa kimataifa walisema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.
Chama hicho cha NPP, kimesema imewasilisha kesi hiyo baada ya kuchunguza takwimu kutoka kwa vituo elfu ishirini na sita vya kupigia kura, vilivyokujwa na zaidi ya kura milioni kumi na moja.
Akufo-Addo alishindwa katika duru ya pili ya uchaguzi wa urais mwaka wa 2008, kwa asilimia moja lakini alikubali matokeo hayo.
Bwna Mahama wa chama cha National Democratic Congress party, alikuwa makamu wa rais wa Ghana hadi kifo cha ghafla cha rais wa hiyo hiyo John Atta Mills, mwezi Julai mwaka huu, ambako aliteuliwa kuhudumu kama kaimu rais wa nchi hiyo.
Taifa la Ghana limekisiwa kuwa nchi iliyo na demokrasia iliyokomaa na thabiti zaidi barani Afrika.
Share:

WAFANYAKAZI WA MAREKANI WAONDOLEWA BANGUI

 28 Disemba, 2012 - Saa 11:57 GMT
Waasi wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati
Waasi wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati
Serikali ya Marekani, imesema imewaondoa raia wake katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, huku waasi wanaopinga serikali wakikaribia kuingia mji mkuu wa nchi hiyo Bangui.
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema haijavunja uhusiano wake wa kibalozi na serikali ya nchi hiyo, ila imechukua tahadhari kuhusu usalama wa raia wake.
Marekani pia imeonya raia wake dhidi ya kwenda nchini CAR wakati wa machafuko hayo.
Hali ya wasi wasi imetanda katika mji mkuu wa Jamuhuri ya Afrika ya kati, Bangui, huku waasi wanaopinga serikali wakikaribia kufika mji huo.
Mjumbe mmoja wa Umoja wa Mataifa ameiambia BBC kuwa ameshuhudia raia wa mji huo wakiwa na wasi wasi mkubwa kutokana na na tishio la shambulio.
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa umewahamisha wafanyakazi wake wote nchini humo, nayo serikali ya Marekani imetoa wito kwa raia wao kuondoka nchini humo.
Serikali ya Ufaransa kwa upande wake imeagiza usalama kuimarisha katika ubalozi wake mjini Bangui, baada ya kushambuliwa na waandamanaji.
Wanajeshi wa Serikali ya CAR
Wanajeshi wa Serikali ya CAR
Waandamanaji hao walirusha mare ya kuchoma bendera ya Ufaransa.
Raia hao wanataka serikali ya Ufaransa kusiadia kuzima uasi Kaskazini mwa nchi hiyo.
Wanadai serikali ya Ufaransa imewatekeleza.
Ufaransa ina takriban wanajeshi mia mbili mjini Banguia na utawala wa nchi hiyo umetoa wito kwa Ufaransa kuingilia kati na kusaidia kukabiliana na wanajeshi wa waasi ambao wameuteka maeneo ya Kaskazini mwa nchi hiyo.
Lakini rais wa Ufaransa Francois Hollande amekataa wito huo.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa ameliambia shirika la Habari la Reuters kuwa mzozo huo unapaswa kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo
Share:

WAHAMIAJI HARAMU WAPATAO 18 WAFARIKI NCHINI MISRI

 28 Disemba, 2012 - Saa 17:36 GMT
Wahamiaji haramu
Wahamiaji haramu wakijaribu kuvuka baharini
Balozi wa Somalia nchini Libya Bwana Abdikani Mohamed Waeys amesema ana taarifa ya vifo vya raia 18 vilivyotokea kutokana na ajali ya lori nchini Libya.
Wasomali hao wanaotajwa kuwa wahamiaji haramu, 23 wameripotiwa kujeruhiwa huku wengine wakiwa katika hali mbaya.
Balozi Abdikani amesema lori hilo lililokuwa limebeba mifuko ya saruji walimokuwa wamejificha Wasomali hao, lilipinduka na kusababisha vifo, na kusema idadi yao walikuwa 120 wakiwemo wanaume na wanawake wote wakiwa ni Wasomali.
Katika miaka ya hivi karibuni idadi ya wahamiaji haramu ambao wamefariki wakijaribu kuvuka baharini imeongezeka.
Share:

Definition List

Unordered List

Support