This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, 23 February 2013

russia ya garagazwa na irani katika mieleka



Timu ya Mieleka ya Iran yatawazwa kuwa mabingwa wa dunia'
 freestyle' baada ya kuigaragaza Russia

Timu ya taifa ya mieleka ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweza kuonyesha uhodari na umahiri wao katika mchezo  wa mieleka baada ya kuibwaga timu ngumu ya Russia kwenye mchezo wa fainali wa kombe la dunia kwa mtindo wa freestyle, baada ya kuibanjua kwa ushindi wa 6 -1, kwenye uwanja wa Azadi mjini Tehran. 
Ikishangiliwa na nyomi za  washabiki elfu kumi na mbili waliofurika uwanjani na wakati wote wa mashindano walikuwa wamesimama wima, huku wakitoa vifijo, nyemi, na hoihoi za  nderemo za Iran, Iran, Iran  na kuwatia morali wanamieleka wa timu ya taifa ya Iran ambao hatimaye walijipatia medali sita za dhahabu katika uzani wa kilo 55, 60, 74, 84, 96 na 120. Hali kadhalika Iran ilijipatia medali ya fedha katika uzito wa kilo 66. Russia iliyoshika nafasi ya pili, iliambulia medali moja ya dhahabu katika uzito wa kilo 66 na medali nyingine sita za fedha.

Timu ya mieleka ya Marekani ilishika nafasi ya tatu na kujizolea medali za shaba baada ya kuibwaga Belarus kwa 6-1. Naye Mkuu wa Shirikisho la Mieleka la Marekani amesema kuwa, watazamaji wa  Iran wameuthibitishia ulimwengu kwamba, Kamati ya Kimataifa ya  Olimpiki IOC ilifanya makosa kwa kuchukua maamuzi ya pupa ya kuufuta mchezo wa mieleka kwenye mashindano ya Olimpiki ya 2020.
Share:

ajali ya ua watu kimi na saba na wengine majeruhi kenya



Watu 17 wauawa kwa ajali ya barabara Kenya
Watu 17 wameuawa leo asubuhi katika ajali mbili tofauti zilizotokea katika
Watu 17 wameuawa leo asubuhi katika ajali mbili tofauti zilizotokea katika maeneo ya Voi na Kilifi katika mkoa wa Pwani nchini Kenya

. Ajali ya Voi iliyahusisha magari mawili ya mizigo na basi la abiria ambapo watu 12 wakiwemo madereva wa magari hayo waliuawa papo hapo.
Imeripotiwa kuwa magari hayo yaliyogongana uso kwa uso yalikuwa yakienda kwa mwendo wa kasi. Ajali ya pili ilitokea katika eneo la Vipingo huko Kilifi ambapo watu 5 walipoteza maisha yao na wengine 14 kujeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyoyahusisha magari mawili ya abiria na watalii. Watu 12 walijeruhiwa kwenye ajali hiyo na kufikishwa kwenye hospitali za maeneo yaliyo karibu kwa matibabu
Share:

serikali ya jk yaongoza kwa kukopa!!!!!


TAASISI isiyo ya kiserikali ina yojishughulisha na masuala ya Madeni ya Taifa na Maendeleo (TCDD), imesema Serikali ya Tanzania ndiyo inaongoza kwa kukopa zaidi, ikieleza kuwa kati ya mwaka 2008 hadi mwaka 2011, imekopa kiasi cha Sh15trilioni na kufanya deni la taifa kufikia Sh21trilioni.


Rais Kikwete aliingia madarakani mwaka 2005, baada ya rais aliye mtangulia, Benjamin Mkapa kumaliza kipindi chake cha uongozi wa miaka 10 kilichoanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2005.
TCDD imebainisha kuwa Serikali inakopa fedha hizo kutoka Benki Kuu (BoT), Benki za Biashara, Kampuni za Bima na Mashirika ya Hifadhi za Jamii. Pia inakopa katika taasisi za kimataifa ikiwamo, Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo Afrika (ADB) na Shirika la Fedha Duniani (IMF).
...........................................................................................................................................................
Share:

Monday, 11 February 2013

wanafunzi 12,000 Dar Hatima haijajulikana


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk Shukuru Kawambwa. 


MKOA wa Dar es Salaam haujakamilisha ujenzi wa madarasa 292 na utengenezaji  madawati 12,000, hivyo kutojulikana hatima ya wanafunzi 11,677 wa chaguo la pili wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu wa masomo.
Hali hiyo imejitokeza baada ya wakurugenzi wa manispaa zote kushindwa kutoa taarifa za maendeleo ya utekelezaji kukamilika kama alivyoagiza  Katibu Tawala wa Mkoa (Rac), Theresia Mmbando.
Mmbando aliagiza wakurugenzi wa manispaa husika,kusimimia ujenzi wa madarasa na utengenezaji madawati na kuwasilisha ripoti ya maendeleo ofisini kwake.
Hata hivyo, hadi mwezi huu hakuna manispaa hata moja ambayo imepeleka taarifa za maendeleeo ya utekelezaji agizo hilo hilo...............
............................................................................................................................................................
Share:

Channel Ten kurusha live mdahalo wa wagombea Kenya

Martha Karua mgombea urais


MDAHALO mkubwa wa wagombea Urais nchini Kenya unafanyika leo na hapa nchini utaonyeshwa moja kwa moja kupitia Kituo cha Channel 10, kwa kushirikiana na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL).
MCL ndio inayomiliki gazeti hili pamoja na yale ya Mwananchi Jumapili, Mwanaspoti, Citizen na Citizen on Sunday.
Watakaoshiriki katika mdahalo huo ni wagombea wa Urais wa nchi hiyo, Raila Odinga, Uhuru Kenyatta, Musalia Mudavadi,  Peter Kenneth, James Kiyiapi, na Martha Karua.
Mdahalo huo utafanyika katika Ukumbi wa Shule ya Kimataifa ya Brookhouse jijini Nairobi kuanzia saa moja usiku.,.....................
.................................................................................................................................................................
Share:

Saturday, 9 February 2013

WANANCHI WAFIKA ZAMBIA KUFUATA UNGA




BAADHI ya wakazi wilayani Nkasi mkoani Rukwa na maeneo mengine ya mwambao wa Ziwa Tanganyika, wamekuwa wakienda nchini Zambia kununua chakula kutokana na tatizo la njaa lililojitokeza katika maeneo hayo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini upatikanaji wa chakula katika eneo hilo umekuwa mgumu kiasi cha kuchangia kupanda kwa bei ya mahindi kufikia Sh180,000 kwa gunia moja.
Mmoja wa madiwani, Privatus Yoramu alisema kuwa hali ya chakula kwenye eneo hilo ni mbaya na iwapo ikiendelea kwa muda wa miezi miwili kama ilivyo hivi sasa upo uwezekano wa familia nyingi kuanza kulala na njaa.........................
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Share:

PINDA AKANWA MKOANI MTWARA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda 


UMOJA wa vyama tisa vya siasa vya upinzani, vinavyoongoza hoja ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara kupinga mradi wa usafirishaji wa gesi kwa njia ya bomba kwenda Dar es Salaam, umekutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kumfikishia ujumbe unaoeleza kuwa wananchi wa Mtwara hawajamwelewa.
Kikao hicho kilifanyika nyumbani kwa Pinda jijini Dar es Salaam, Jumamosi ya Februari 2, baada ya umoja huo kukosa nafasi ya kukutana naye kwa mara ya pili, wakati Waziri Mkuu huyo alipofanya majumuisho ya ziara yake mkoani Mtwara katika Ukumbi wa Veta mjini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mtwara jana, mmoja wa wajumbe wa umoja huo Mustafa Nchia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Mtwara Mjini, alisema kuwa walilazimika kufunga safari kwenda kuonana na Waziri Mkuu, ili kumfikishia ujumbe kuwa wananchi wa Mtwara bado hawajamwelewa.

“Tulikutana Jumamosi nyumbani kwake Dar es Salaam, tukamwambia kuwa wananchi wa Mtwara bado hawajakuelewa… Baada ya kumaliza ziara yake katika majumuisho hakutuuliza kama tumekubaliana au la,” alisema Nchia na kuongeza:,,,,,,,,
................................................................................................................................................................
Share:

Wednesday, 6 February 2013

Elimu yenye matabaka hujengwa na watu katika jamii





MATOKEO mazuri au mabaya  ya elimu kwa mtu,  huonekana katika namna anavyotenda mambo na dhamira yake ya kutenda,  na wala hayatokani na alichojifunza, namna alivojifunza na sababu ya kujifunza.
Hiyo ndio tofauti kubwa kati ya shule yenye kutoa maarifa na ujuzi na shule yenye kutoa vyeti na sifa za kumuwezesha mtu kupata kazi.
Watu wengine wanapozungumzia elimu wanafikiri kuhusu utaratibu mzima wa kujifunza wenye lengo la kumpatia mtu ujuzi na maarifa na kumudu vyema kile alichojifunza.
Ujuzi na maaarifa ndio hasa lengo na upatikanaji wake  unaotarajiwa utumike katika kupambana na changamoto na hata kuibua na kuleta maarifa mengine zaidi.
Kuna watu wengine wanapozungumzia elimu,  wanafikiria umiliki wa cheti kinachoonyesha una ujuzi fulani.
Elimu ya aina hii sio kwa ajili ya kutumika katika maisha wala kutafuta maarifa mengine,  bali ni kwa ajili ya mtu kukariri anachojifunza na  kuyatoa yale maarifa yaliyokaririwa katika mitihani ili apate cheti kizuri kitakachowezesha kupata kazi yenye kipato kizuri....................................
.
Share:

Tuesday, 5 February 2013

Raia sita waua Afghanistan na Askari wa Marekani

Askari wa Marekani waua raia sita Afghanistan
Askari wa muungano wa vikosi vya kigeni wanaoongozwa na Mareakani nchini Afghanistan, wamewaua raia sita katika jimbo la Herat huko magharibi mwa nchi hiyo.
 Kiongozi mmoja katika jimbo hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa, wahanga wote wa mashambulizi hayo ya askari wa kigeni, ni watoto na wanawake.
 Viongozi wa usalama nchini Afghanistan wamesema kuwa, mauaji hayo yamejiri katika mapigano kati ya wanamgambo na askari hao wa kigeni katika jimbo hilo. Katika mashambulizi hayo, wanamgambo wengine 10 wameripotiwa kuuawa.
Hii sio mara ya kwanza kwa askari hao wa kigeni wanaoongozwa na Marekani kutekeleza mauaji dhidi ya raia wasio na hatia wa Afghanistan, suala ambalo limezidisha chuki na hasira kali kwa jamii ya Waafghani dhidi ya Marekani. Marekani na waitifaki wake iliivamia Afghanistan kwa madai ya kupambana na ugaidi, uvamizi ambao ulipelekea kuung’oa madarakani utawala wa Wataleban.
 Hata hivyo pamoja na kupita kipindi cha miaka 11 wavamizi hao hawajaweza kurejesha hali ya usalama na amani nchini humo.
Share:

Monday, 4 February 2013

Wanamgambo wa Boko Haram 17 wauawa huko Borno Nigeria

  

 Boko Haram 17 wauawa huko Borno Nigeria
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, limewauwa wanamgambo 17 ambao ni wanachama wa kundi la Boko Haram katika jimbo la Borno, baada ya kujiri mapigano baina ya pande mbili kaskazini mashariki mwea nchi hiyo.
  Luteni Kanali Sagir Mussa Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema kuwa, mwanajeshi mmoja wa serikali amepoteza maisha yake katika mapigano hayo makali. Ameongeza kuwa, vituo viwili vya utoaji mafunzo vya wanamgambo wa Boko Haram vimeharibiwa kabisa na majeshi ya serikali ya Nigeria katika jimbo hilo la Borno. Hayo yanajiri katika hali ambayo, serikali ya Nigeria imesema kuwa ipo tayari kuangalia pendekezo lililotolewa na kundi la Boko Haram la kusitisha mapigano

. Makamu wa Rais wa Nigeria Namadi Sambo amenukuliwa hivi karibuni akisema kuwa, Abuja inakaribisha pendekezo hilo la usitishaji mapigano la Boko Haram na kwamba serikali itajitahidi kuhakikisha kwamba amani inapatikana nchini humo. Kundi Boko Haram limehusika katika milipuko na mashambulizi tofauti katika miji kadhaa ya Nigeria tangu mwaka 2009.  Zaidi ya watu 1000 wameuawa katika mashambulizi ya kundi hilo kuanzia mwaka 2009.
Share:

muundo mpya wa serikali ya CAR wapingwa na Waasi waSeleka

 

Seleka wapinga muundo wa serikali mpya CAR
Waasi wa Seleka wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wametangaza kuwa wanapinga muundo wa serikali mpya ya nchi hiyo iliyotangazwa hapo jana ikiwa ni matunda ya makubaliano ya amani ya Libreville Gabon. Taarifa ya waasi hao imebainisha kwamba, haiitambui serikali hiyo kutokana na kupatiwa hisa ndogo mno

. Waasi wa Seleka wamesisitiza kuwa, Waziri Mkuu mpya wa nchi hiyo amepuuza mapendekezo yote ya waasi hao katika kuteuwa mawaziri wa serikali mpya. Taarifa iliyotolewa na waasi hao muda mchache tu baada ya kutangazwa serikali mpya ya umoja wa kitaifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati imesisitiza kuwa, waasi hao wanataka kupatiwa wizara saba hadi nane katika serikali hiyo mpya.
Serikali mpya ya Jamhuri ya Afrika ya Kati ina wizara 32 ambapo vyama vya upinzani na muungano wa waasi wa Seleka huko Jamhuri ya Afrika ya Kati vimechukua wizara muhimu zikiwezo za fedha na madini katika serikali mpya iliyotangazwa ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya amani yaliyofikiwa kati ya serikali na wapinzani.
 Na Salum Bendera
Share:

Friday, 1 February 2013

Maombi kufunguliwa Kanisa Dar Mahakama yatupa


Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi  wa Ilala,Duwani Nyanda

Akizungumza na viongozi  wa Kanisa la MMAHAKAMA Kuu Kitengo cha Ardhi Dar es Salaam, imetupilia mbali ombi  la  Bodi ya Wadhamini ya Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini, la kutaka kufunguliwa makufuli yaliyofungwa katika Kanisa la Usharika wa Tabata, ili waweze kumsimika mchungaji mpya, ambaye ni Lawi Mwankuga.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Mathew Mwaimu,baada ya bodi  hiyo ya wadhami wa Kanisa la Moravian Kusini chini ya Mchungaji Clement Mwaitebele, kupitia wakili wao, Henry Chaula wa Kampuni ya Uwakili ya C&M,  kufungua kesi namba 12  ya mwaka 2013 na kuomba isikilizwe chini ya  hati ya dharura.
Kwa mujibu wa kesi hiyo, Mchungaji Gervas Mwakafwila, Mchungaji Silas Mwakibinga, Tukuswiga Mwakabur, Atuganile Mbombo, Isakwisa Ernest  na Sekela Mukisele  ambao wanatetewa na Wakili
  Benjamin Mwakaganda wa Kampuni ya uwakili ya  BM,  wanadaiwa  kufunga makufuli kwenye  Kanisa la Usharika wa Tabata, ili kuzuia bodi hiyo  kumsimika mchungaji mpya..................................
.........................................................................................................................................................

Share:

Definition List

Unordered List

Support