Saturday, 23 February 2013

russia ya garagazwa na irani katika mieleka



Timu ya Mieleka ya Iran yatawazwa kuwa mabingwa wa dunia'
 freestyle' baada ya kuigaragaza Russia

Timu ya taifa ya mieleka ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweza kuonyesha uhodari na umahiri wao katika mchezo  wa mieleka baada ya kuibwaga timu ngumu ya Russia kwenye mchezo wa fainali wa kombe la dunia kwa mtindo wa freestyle, baada ya kuibanjua kwa ushindi wa 6 -1, kwenye uwanja wa Azadi mjini Tehran. 
Ikishangiliwa na nyomi za  washabiki elfu kumi na mbili waliofurika uwanjani na wakati wote wa mashindano walikuwa wamesimama wima, huku wakitoa vifijo, nyemi, na hoihoi za  nderemo za Iran, Iran, Iran  na kuwatia morali wanamieleka wa timu ya taifa ya Iran ambao hatimaye walijipatia medali sita za dhahabu katika uzani wa kilo 55, 60, 74, 84, 96 na 120. Hali kadhalika Iran ilijipatia medali ya fedha katika uzito wa kilo 66. Russia iliyoshika nafasi ya pili, iliambulia medali moja ya dhahabu katika uzito wa kilo 66 na medali nyingine sita za fedha.

Timu ya mieleka ya Marekani ilishika nafasi ya tatu na kujizolea medali za shaba baada ya kuibwaga Belarus kwa 6-1. Naye Mkuu wa Shirikisho la Mieleka la Marekani amesema kuwa, watazamaji wa  Iran wameuthibitishia ulimwengu kwamba, Kamati ya Kimataifa ya  Olimpiki IOC ilifanya makosa kwa kuchukua maamuzi ya pupa ya kuufuta mchezo wa mieleka kwenye mashindano ya Olimpiki ya 2020.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Definition List

Unordered List

Support