| Waandishi wa habari 74 wuawa Amerika ya Latini |
Asasi moja isiyo ya kiserikali
imeripoti kuwa, kwa akali waandishi wa habari 74 wameuawa katika kipindi
cha miaka mitatu iliyopita katika eneo la Amerika ya Latini. Asasi hiyo
inayohusika na utetezi wa uhuru wa vyombo vya habari na magazeti katika
eneo la Amerika ya Latini imeeleza kuwa, nchi za Mexico na Honduras ni
hatari zaidi kwa usalama wa waandishi wa habari na katika kipindi cha
miaka mitatu iliyopita. Kwa uchache waandishi wa habari 49 waliuawa
katika nchi hizo mbili. Taasisi hiyo imeeleza kuwa, waandishi wa habari 9
wameuawa nchini Brazil, na wengine saba nchini Ecuador. Taarifa hiyo
imeongeza kuwa, waandishi wengine sita waliosalia wameuawa katika nchi
za Peru, Colombia, Guatemala na Argentina.






0 comments:
Post a Comment