Friday, 13 September 2013

UNHCR - Tanzania haijawafukuza wakimbizi

 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, ofisi ya Tanzania limekanusha taarifa katika baadhi ya vyombo vya habari kwamba, Tanzania imewarejesha nyumbani kwa nguvu, wakimbizi 25,000 wa Burundi mwezi mmoja uliopita.

Vilevile serikali ya Tanzania imesema, taarifa hiyo ni ya uzushi ambayo haina ukweli wowote na yenye nia ya kuichafulia jina nchi ya Tanzania ambayo kwa muda mrefu imekuwa kimbilio na makazi ya wakimbizi wengi kutoka nchi mbalimbali hasa za Ukanda wa Maziwa Makuu.

Akizungumza na BBC, Mwakilishi Mkazi wa UNHCR nchini Tanzania , Bi. Joyce Mends Cole, amesema, amewasiliana na mwakilishi wa shirika hilo nchini Burundi ambaye amethibitisha kwamba hakuna wakimbizi wa nchi hiyo waliorejeshwa kutoka Tanzania.
Share:

1 comments:

Definition List

Unordered List

Support