Monday, 11 February 2013

wanafunzi 12,000 Dar Hatima haijajulikana


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Dk Shukuru Kawambwa. 


MKOA wa Dar es Salaam haujakamilisha ujenzi wa madarasa 292 na utengenezaji  madawati 12,000, hivyo kutojulikana hatima ya wanafunzi 11,677 wa chaguo la pili wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu wa masomo.
Hali hiyo imejitokeza baada ya wakurugenzi wa manispaa zote kushindwa kutoa taarifa za maendeleo ya utekelezaji kukamilika kama alivyoagiza  Katibu Tawala wa Mkoa (Rac), Theresia Mmbando.
Mmbando aliagiza wakurugenzi wa manispaa husika,kusimimia ujenzi wa madarasa na utengenezaji madawati na kuwasilisha ripoti ya maendeleo ofisini kwake.
Hata hivyo, hadi mwezi huu hakuna manispaa hata moja ambayo imepeleka taarifa za maendeleeo ya utekelezaji agizo hilo hilo...............
............................................................................................................................................................

Hatua hiyo inamaanisha wanafunzi wa chaguo la pili, hawatajiunga kidato cha kwanza kama ilivyopangwa hado miundombinu hiyo itakapokamilika.
Akizungumza kwa simu juzi,  Ofisa Habari Mkoa wa Dar es Salaam, Adrophina  Ndyeikiza alikiri kutopokelewa kwa ripoti hizo kutoka kwa wakurugenzi wa manispaa.
“Mpaka sasa hakuna ripoti yoyote kutoka kwa wakurugenzi, lakini nadhani zitakuwapo katika taarifa yetu ya kujitathmini ambayo tunatarajia kuitoa baada ya muda mfupi. Nadhani wiki ijayo taarifa itatoka ambayo itajumuisha ripoti zote,” alisema Ndyeikiza.
Wanafunzi 51,433 sawa na asilimia 88.54 walifaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu, kati yao 39, 756 walichaguliwa chaguo la kwanza kulingana na miundombinu uliyopo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Definition List

Unordered List

Support